Mwanamuziki kutoka nchini Burundi anayetambulika kwa jina la Masterland ameuvisha taji mpya muziki wa Buja fleva masaa machache tu baada ya kuachia wimbo wake mpya ambao umeambatana na video kwa pamoja.
Baada ya kuwa amewaahidi mashabiki na wanaofuatilia sana muziki wa nyumbani kwa kipindi cha mwezi mmoja kuwa ataachia wimbo huo,tayari sasa amaeikamilisha ahadi yake.
Video ya wimbo huo uliopewa jina la NTUNDEKURE inadaiwa tubeba gharama isiyopua kiasa cha Faranga 4.000.000 fbu kupanda,kama alivyo sema yeye mwenyewe siku ya jana kipindi anahojiwa na watangazaji na baadhi ya watu ambao walikuwa wamehudhuria.
Cha kujivunia kwenye wimbo huo na video yake,ni kwamba baadhi ya watu ambao washaiona tayari wanasema kuwa ni hatua kubwa sana kwa muziki wa Burundi maana wanasema kuwa video hiyo ni mara ya kwanza kuonekana Burundi wengine wanakwambia kuwa hata kwenye nchi jirani na Burundi video hiyo haijapaonekana maana ubora na mvuto wake hauna kipimo.
Nafasi na kazi ni vyoko ndugu msomaji wa habari hii.
Sikiliza na pakua(download) wimbo huo hapa.
Tazama video hiyo hapa.usisahau kuwashirikisha wenzako.
Podcast: Play in new window | Download (Duration: 3:10 — 5.1MB)
Subscribe: Apple Podcasts | Email | RSS
Comments