Search in the website:

HABARI ZA ULIMWENGU / Page 2

Kiongozi wa upinzani ashinda uchaguzi wa urais Ghana

10 décembre 2016

Mwanasiasa mkongwe ameshinda uchaguzi wa urais nchini Ghana, ushindi ambao umepokelewa kwa shangwe na nderemo na wafuasi wake. Nana Akufo-Addo, alishangilia ushindi wake na kusema taifa hilo sasa ni mwenge wa demokrasia Afrika Magharibi. Ameahidi kukabiliana na uchumi uliozorota, swala ambalo lilitiliwa mkazo wakati wote wa kampeni, Bw Akufo-Addo alisema kuwa ushindi wake ni hatua […]

Read More

Raia wawili wa Iran wakamatwa wakipiga picha Kenya Nairobi

1 décembre 2016

Gazeti la Daily Nation la nchini Kenya linasema kuwa raia wawili wa Iran wamekamatwa kwenye mji mkuu Nairobi. Watu hao ni kundi la pili la raia wa Iran kukamywa nchini Kenya kwa ushukiwa kunpanga njama ya kutaka kufanya mashambulizi ya kigaidi. Mwezi Juni mwaka 2012 utawala nchini Kenya uliwakamata Ahmad Mohammed na Sayed Mousavi wa […]

Read More

Sababu za kuanguka kwa ndege ya Brazil zatajwa

1 décembre 2016

Ndege iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya mpira kutoka nchini Brazil ambayo ilipata ajali nchini Colombia inasemekana kwa muujibu wa taarifa zilizovuja ndege hiyo iliishiwa mafuta kutoka katika kifaa cha kurekodia mawasiliano. Katika mnara wa mawasiliano ya ndege , rubani alisikika akirudia mara kadhaa akiomba ruhusa ya kutua kwa dharura kutokana na hitilafu ya umeme […]

Read More

Raia wa Gambia wapiga kura za urais na ubunge

1 décembre 2016

Wapiga kura katika taifa la magharibi mwa Afrika Gambia wanaelekea katika uchaguzi ambao rais aliyepo mamlakani Yahya Jammeh anasema kuwa atashinda. Rais Jammeh ambaye alichukua mamlaka katika mapinduzi ya mwaka 1994 anasema kuwa ataongoza kwa miaka bilioni Allah akipenda. Akiwania wadhfa huo kwa muhula wa tano amesema kuwa anapiga marufuku maandamano baada ya uchaguzi huo […]

Read More

Donald Trump asema kuwa Fidel Castro alikuwa ‘dikteta katili’

26 novembre 2016

Rais Mteule wa Marekani Donald Trump amesema kiongozi wa zamani wa Cuba Fidel Castro alikuwa «dikteta katili» saa chache baada ya Bw Castro kufariki dunia akiwa na miaka 90. Bw Trump amesema: «Leo, ulimwengu umeshuhudia kifo cha dikteta katili aliyewakandamiza watu wake kwa karibu miongo sita. Utawala wake ulikuwa wa watu kuuawa kwa kupigwa risasi, […]

Read More

Tarehe muhimu za kukumbuka kuhusu Fidel Castro

26 novembre 2016

1926: Azaliwa mkoa wa kaskazini mashariki wa Oriente nchiniCuba 1953: Afungwa jela baada ya kuongoza maasi ambayo hayakufanikiwa dhidi ya utawala wa Batista 1955: Aachiliwa huru kutoka jela chini ya mkataba wa msamaha 1956: Akiwa na Che Guevara, aanza vita vya kuvizia dhidi ya serikali 1959: Amshinda Batista, na kuapishwa waziri mkuu wa Cuba 1961: […]

Read More

Fidel Castro kiongozi wa zamani wa Cuba aliyeongoza mapinduzi ya Kikomunisti afariki dunia akiwa na miaka 90

26 novembre 2016

«Amiri jeshi mkuu wa mapinduzi ya Cuba alifariki dunia mwendo wa saa 22:29 usiku huu (03:29 GMT Jumamosi),» Rais Raul Castro ametangaza. Fidel Castro alitawala Cuba kama taifa la chama kimoja kwa karibu miaka 50 kabla ya kakake Raul kuchukua hatamu 2008. Wafuasi wake walisema alikuwa ameirejesha Cuba kwa wananchi. Lakini alituhumiwa pia kwa kuwakandamiza […]

Read More

Clinton na Trump watifuana vikali kwenye mdahalo wa pili wa Urais Marekani

11 octobre 2016

Mdahalo wa pili wa Urais nchini Marekani, umefanyika Jumapili hii huko St Louis, Missouri. Wagombea, Donald Trump na Hillary Clinton walitabasamiana lakini hawakushikana mikono walipotambulishwa jukwaani. Mdahalo huo ulianza kwa mjadala iwapo Trump anafaa kuwa amri jeshi mkuu kulingana na jinsi anavyowazungumzia wanawake. Alirudia kile alichokisema baada ya video ya mwaka 2005 inayomuonesha akiongea maneno […]

Read More

Watu 21 wauawa katika shambulizi kusini mwa Sudan Kusini

11 octobre 2016

Watu ishirini na moja, wengi wao wakiwa wanawake na watoto, waliuawa Jumamosi katika shambulizi lililohusishwa waasi wa Sudan Kusini kwenye barabara inayotokea mji mkuu, Juba, katika mji wa Yei, kusini mwa Sudan Kusini inayokumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu mwishoni mwa mwaka 2013, polisi imetangaza Jumatatu hii. Lori lililokua likisafirisha raia walioyakimbia makazi […]

Read More

Rais wa Haiti aelezea kuhusu madhara ya kimbunga Matthew

11 octobre 2016

Rais wa mpito nchini Haiti, Jocelerme Privert amesema kuwa kimbunga Matthew kimeleta uharibifu mkubwa wa miuondombinu na mauaji ya watu wengi. Amesema kuwa wananchi wa Haiti wanahitaji maji, chakula na dawa haraka sana na mipango ya muda mrefu inahitajika ili kuzuia njaa kuendelea. Ameongeza kuwa siasa za Haiti zinahitaji kurekebishwa. Uchaguzi wa Urais nchini humo […]

Read More

Load more

Share
Share